Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan endapo atashinda, amewaahidi wafugaji katika wilaya ya Tun duru iwapo watamchagua katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 ataendeleza sekta ya mifugo kwa kuhakikisha inakuwa na tija zaidi kwa wafugaji.
Hata hivyo mgombea huyo amesema serikali ya CCM ikichaguliwa itaendelea kutoa chanjo kwa mifugo, kujenga mashosho na minada ya kisasa, pamoja na kuboresha mabucha ili nyama inayofika sokoni iwe salama na yenye ubora. Katika hatua nyingine Mhe. Dkt.Samia , ameahidi kutenga vitalu 221 maalum kwa ajili ya shughuli za ufugaji, hatua itakayowapa wafugaji mazingira bora ya kuzalisha na kuongeza tija katika shuguli za ufuagaji.

